IDARA YA UMEME YANUFAIKA NA MAFUNZO YA VIFAA TIBA.

2025-02-21 12:29:56 category

TAASISI ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST), kupitia Idara ya Umeme, leo tarehe 21/02/2025, imefunga mafunzo kuhusu utumiaji wa Vifaa mbali mbali vya kufundishia Wanafunzi wanaosoma fani ya Electrical and Biomedical Engineering.

Mafunzo hayo yametolewa na  Profesa Daniel Lawrence Schuster kutoka Taasisi ya BETA Aid (Biomedical Engineering Technology Aid) iliopo nchini Marekani, ambapo mafunzo hayo yamefanyika katika Workshop ya Electrical and Biomedical Engineering katika Taasisi ya Karume Mbweni Zanzibar.

Jumla ya Wakunzi watano (5), wamepata mafunzo hayo na kupatiwa Vyeti vya Ushiriki wa Mafunzo  ambayo yaliendeshwa kwa muda wa wiki mbili.